Tuesday, June 12, 2012
NENO LA KUTIA NGUVU ASUBUHI YA LEO: KASIMAME IMARA !!!
Inawezekana dunia imekupiga dafrau mpaka umefikia kuona kuwa maisha yako haya maana yo yote hapa duniani.
Inawezekana jamii imekuaminisha kuwa wewe ni mnyonge na kefule tu asiye na matumaini yo yote wala kesho yenye utukufu
Asubuhi ya leo nakuomba usimame wima na kuukana uwongo huu ulioshindiliwa ndani mwako kwa muda mrefu na mifumo gandamizi ya kijamii kiasi cha kukuondolea mng'aro wako na kukugeuza kuwa mpapasi tu asiyejua aendako.
Haupo hapa duniani kwa bahati mbaya na ukichunguza vizuri utaliona lengo na kusudio lako lililokufanya uje hapa duniani. Maisha yako yana maana na thamani sawasawa na ya binadamu mwingine ye yote - awe tajiri kupindukia, msomi aliyebobea, mtu mwenye umashuhuri wa kuandamwa kila aendako.....
Nyanyua shingo yako kama afanyavyo twiga - yule mnyama mlimbwende mpole na mwenye madaha. Jitahidi uone mbali zaidi kuliko wengine. Kaitazame dunia kwa jicho jipya. Nenda ukapambane !!!
Masangu Matondo Nzuzullima (MMN) at Tuesday, June 12, 2012
Share
Mija Shija SayiJune 12, 2012 at 8:20 AM
Yaani wamarekani wako mbali sana katika maneno ya kutia moyo...
Kaka Matondo nashukuru sana kwa kipengele hiki maana mimi ni mdhaifu sana wa waneno yakutia moyo, yaani nayapenda sana.
Baraka kwako na familia.
Reply
Replies
Masangu Matondo Nzuzullima (MMN)June 12, 2012 at 7:25 PM
Da Mija;
Nimejifunza kuhusu kuanza kila siku kwa mtazamo chanya. Japo njia ya kawaida ni kutumia mafungu ya Biblia pamoja na maombi, hata maneno ya kawaida tu kama haya yanaweza kuwa na athari nzuri.
Basi pita hapa kila asubuhi kuyapata maneno haya ya kutia moyo.
Salami kwako pia, Manjula na familia yote. Mbarikiwe !!!
Reply
Yasinta NgonyaniJune 12, 2012 at 11:01 AM
Kaka Matondo ahsante kwa kutushirikisha katika maneno haya kwani nadhani tunahitaji kukumbushana na kutiana moyo. Nimeyapenda. Aamani Daima.
Reply
Replies
Masangu Matondo Nzuzullima (MMN)June 12, 2012 at 7:33 PM
Asante Da Yasinta...
Dunia hii inachosha na ni rahisi sana kukata tamaa. Kumbe tungejua watu wengine wanapambana na shida kubwa zaidi kuliko zetu, tungejikakamua na kushukuru hata kwa kuweza tu kuamka leo asubuhi tukiwa wazima na salama.
Kutiana moyo - hata kwa njia hii tu inaweza kutukumbusha kuyatazama mambo katika uzuri wake na siyo kulalamikia ubaya tu utafikiri kwamba ubaya na matatizo vimejitenga na mfumo mzima wa mambo.
Reply
AnonymousJune 18, 2012 at 12:07 PM
Asante kaka Matondo kwa hili. Nimepita hapa uani kwako baada ya muda mreeeeefuuu. Na leo , nimeamka nikiwa nimedorora vibaya sana kwa mawazo lukuki na kila siku kujihesabia mikosi na bahati mbaya.
Nadhani umetumika kunitia moyo maana nilikuwa napiga mwayo hadi ukaishia nusu. Najihisi tofauti ghafla na maneno ni ya kawaida sana lakini yamekuja kwa wakati!
Saingine tunasahau kuhesabu baraka ( Kwizukwa mbango).
Asante for this
Kipapli
Reply
Replies
Masangu Matondo Nzuzullima (MMN)July 16, 2012 at 8:06 AM
Asante ndugu yangu. Ni rahisi sana kujikita katika uhasi na kusahau mema na mibaraka tuliyonayo. Kumbe hata ile kuweza kuamka tu kitandani ni mibaraka tosha.
Tuendelee kutiana moyo ili tuweze kusonga mbele na safari yetu.
Mungu Aendelee kukubariki wewe na familia yako. Ikalagi mhola badugu bane !!!
AnonymousApril 4, 2013 at 12:09 PM
Prof.Dickison Kamgisha tuwasiliane kwa no.+0743592888, Kamgisha(x-Shidusa Chairman)
Reply
Links to this post
Create a Link
‹
›
Home
View web version
Sikuwahi kuamini kitu kama hiki kingeweza kunitokea hadi ndoa yangu ilipokaribia kuisha kabisa.
JibuFutaMume wangu alibadilika ghafla. Mwanaume ambaye hapo awali alinipenda na kunijali akawa baridi, asiyejali, na mwenye hasira bila sababu. Aliacha kuonyesha nia katika ndoa yetu, akaniepuka kabisa, na hatimaye akaniomba talaka. Nilivunjika moyo kwa sababu nilimpenda mume wangu kwa moyo wangu wote.
Mambo yalizidi kuwa mabaya aliponizuia kila mahali — WhatsApp, Facebook, Instagram — kana kwamba sijawahi kuwepo. Nililia kila usiku nikijiuliza nilifanya nini kibaya.
Siku moja, rafiki wa karibu alinitembelea na kunitambulisha kwa mtu wa kiroho anayeitwa Dkt. Dawn. Kwa kweli, mwanzoni nilikuwa na shaka, lakini niliamua kumweleza kila kitu kwa sababu sikuwa na chochote cha kupoteza.
Dkt. Dawn alinisomea mambo ya kiroho, na nilishtuka. Alifichua siri kuhusu ndoa yangu na maisha yangu binafsi ambayo hakuna mtu aliyejua. Kila kitu alichosema kilikuwa sahihi 100%. Kisha akafichua kwamba mwanamke mwingine alikuwa amemloga mume wangu. Mwanamke huyu alikuwa akimtembelea mara nyingi, na kwa upumbavu niliamini ilikuwa kuhusu kazi tu.
Dkt. Dawn alinisaidia kuvunja uchawi na kufanya ibada yenye nguvu ya kurejesha upendo kwa ndoa yangu.
Kwa mshangao wangu mkubwa, muda mfupi tu baadaye, mume wangu alinifungulia kizuizi mwenyewe na kuanza kunipigia simu na kunitumia ujumbe mwingi, akiniomba nimsamehe na nirudi nyumbani. Mwanzoni nilimpuuza kwa sababu ya maumivu aliyonisababishia, lakini hatimaye alirudi nyumbani akiwa na zawadi na machozi machoni mwake akiomba nafasi nyingine.
Leo, ndoa yetu ni imara zaidi, yenye furaha zaidi, na yenye amani zaidi kuliko hapo awali. Mapenzi kati yetu yanahisi upya kabisa.
Kana kwamba hiyo haitoshi, Dkt. Dawn baadaye alinisaidia na ibada ya ujauzito kwa sababu tulikuwa tumejitahidi kwa miaka mingi kupata watoto. Ndani ya wiki 8, nilipata mimba kiasili, na leo tumebarikiwa na wavulana wawili wazuri wenye afya njema.
Nitaendelea kushukuru milele.
Ukihitaji: Uchawi wa mapenzi ili kuungana tena na mpenzi wako wa zamani
. Usaidizi wa kurejesha ndoa
. Tamaduni za ujauzito ili kupata mimba
. Usaidizi wa kiroho kwa kesi za mahakamani au kupona urithi
. Mwongozo na ulinzi wa kiroho
. kutokuwa na uhakika wa ubaba au ubaba usio na sifa
Ninapendekeza sana Dkt. Dawn. Ushuhuda wangu ni wa kweli, na furaha yangu leo ni uthibitisho. WhatsApp yake: +2349046229159
Email dawnacuna314@gmail.com