Tafuta katika Blogu Hii

Jumatatu, 10 Julai 2017

Mume Wangu Hanitoshelezi Kitandani-Now I’m Sleeping With My ex'' - lady

Mume Wangu Hanitoshelezi Kitandani-Now I’m Sleeping With My ex'' - lady

Kamgisha Blog / 46 minutes ago

Hello, please post this as you might just be helping me save my future.

My name is Daisy. I’m 25 and might be getting married in December, if only I will say yes to my man.

He’s 31 by the way, but I told him I was going to think about it. To cut the story short, I’m really scared of getting married to him because I wouldn’t want to cheat on my husband. This guy is not even a one minute man when it comes to scx. He is a 5 seconds person. I’ve complained severally and he has tried to take all kinds of drugs to make him last but they don’t work.

Whenever we are ready to get down and he is inside me, he just thrusts for 5 seconds and that’s it. Then he leaves me wanting and he can’t go a second round because his body can’t do it. There was a time I was so horny, I had to go meet my ex and yes he made me feel like a woman. But with my soon to be hubby I don’t feel that way. He does not smooch me, he just goes straight in and then everything is over in a blink. I’m just frustrated and I need advice because he has tried basically every solution including Viagra, but the after effect was bad.

How can I be a faithful wife after I get married to this guy when he can’t even satisfy my urge? What should I do?

Visit website

Tebelea hopo kujionea

https://youtu.be/LSuh3TMMWPo

Jumapili, 9 Julai 2017

Zimbabwe yatwaa Kombe la Cosafa

Zimbabwe yatwaa Kombe la Cosafa

KAMGISHA BLOG / 10 hours ago


Timu ya Taifa ya Soka ya Zimbabwe imetwaa ubingwa wa mashindano ya COSAFA2017 baada ya kuifunga Zambia mabao 3-1


Magoli ya Zimbabwe yalitiwa wavuni na  22' K. Mutizwa, 57' T. Chawapiwa pamoja na 67' O. Mushure

Huku goli moja la Zambia kifungwa na 39' L. Mundia

Mambo 10 ambayo ni Sumu katika Mapenzi

Mambo 10 ambayo ni Sumu katika Mapenzi

KAMGISHA BLOG / 9 hours ago

KATIKA harakati zako za kutafuta mpenzi, unaweza kukutana na mwanamke ambaye kwa sababu moja au nyingine anakwondolea uwezo wako wa kufikiri, kutumia mantiki na pia kutumia akili yako ya kuzaliwa. Si lazima awe amekufanyia kitu, lakini inaweza kuwa ni ulevi wako tu unaosababisha ufanye mambo yasiyo ya kawaida. Pengine ndiyo maana baadhi ya wasanii huzungumzia suala la “kudata” kutokana na mapenzi.

Ni jambo jema kudhani kuwa wewe na mpenzi wako mnapendana kwa dhati na kwamba kila mmoja amefika kwa mwenzake, lakini kama mojawapo ya mambo haya kumi yaliyoelezwa hapa chini litajitokeza, basi fahamu kuwa yamkini umependa kuliko kawaida, yaani ni kama umenyweshwa sumu ya penzi. Kumbuka kupenda ni kuzuri, lakini kupenda kupindukia kunaweza kukutumbukia nyongo, kwani katika kila jambo kinahitajika kiasi.

1. WIVU WA KUPINDUKIA
Ni jambo jema kwa mwanamume kumtakia heri mpenzi wake na kufanya kila awezalo kuhakikisha kuwa hapati madhara, lakini iwapo utakuwa mtu wa wasiwasi na mashaka pale unapomwona mpenzi wako akizungumza na mwanamume mwingine, au anapotoka na marafiki zake wa kike, au anapovaa nguo inayomfanya atamanishe, basi fahamu kuwa tayari umekunywa sumu ya mapenzi.

Katika uhusiano wa kimapenzi, kuaminiana ni jambo muhimu sana. Kama kweli unataka mpenzi wako akupende kwa dhati, mwoneshe kuwa unamwamini na unaheshimu maamuzi yake, ikiwa ni pamoja na maamuzi ya kutoka na marafiki zake wa kike na kuwa na marafiki wa kawaida wa kiume. Ondoa hofu na acha kabisa kumpeleleza, maana wapo wanaume ambao hutumia muda wao mwingi kuwapeleleza wapenzi wao ikiwa ni pamoja na kuwategeshea kamera na rekoda za simu.

2. KUTOMWACHIA NAFASI MPENZI
Kama huishi na mpenzi wako ni jambo la kawaida kuwa na hamu ya kumwona mara kwa mara, lakini kumbuka kuwa mpenzi wako naye ana maisha yake na anahitaji nafasi ya kuwa peke yake kwa ajili ya mambo yake binafsi.

Hisia za kutaka kuwa na mpenzi wako muda wote zinaweza kudhaniwa kuwa ni za mapenzi ya dhati, lakini kwa hakika hiyo si ishara njema ya mapenzi ya kudumu. Hebu jiulize kama unaweza kuendeleza hali hiyo maisha yako yote. Ni wazi kuwa utachoka. Kwa hiyo, mpe mpenzi wako fursa ya kupumua. Namna hii mpenzi wako atajenga hamu ya kutaka kukutana nawe lakini ukiwa naye muda wote hamu hiyo itaisha.

3. KUMWAMULIA MPENZI MAMBO YAKE
Unaweza kujikuta ukisukumwa kumwambia mpenzi wako awe anavaa nini wakati gani, akutane na nani na kwa wakati gani au ale nini. Ukiona hivyo, fahamu kuwa hayo si mapenzi, bali umepitiliza na pengine mwisho wa uhusiano wenu unanukia.

Hata ukiachilia mbali suala zima la usawa wa jinsia, hakuna mwanamke ambaye angependa apangiwe kila kitu kuhusiana na maisha yake. Kama ilivyodokezwa hapo juu, kila mtu ana maisha yake na kilichowaunganisha ni mapenzi tu. Kama utataka kumpangia kila kitu ni wazi kuwa utaishia kuishi peke yako.

4. KUMUULIZA MPENZI MASWALI
Iwapo utajikuta ukimuuliza mpenzi wako maswali mengi yanayoonesha wasiwasi wako kuhusiana na mwenendo wake, fahamu kuwa kuna tatizo na tatizo hilo lisipopatiwa ufumbuzi utakuwa mwanzo wa mwisho wa uhusiano wenu.

Mwanamke angependa umuulize maswali ya kawaida kuhusiana na jinsi siku yake ilivyokuwa na kama marafiki zake hawajambo au la, lakini kila jambo lina mpaka wake. Mwanamke hatarajii kuwa kila mnapokutana atakuwa kama ameingia kwenye chumba cha mtihani au usaili wa kazi.

5. KUTOAMINI ANACHOKWELEZA MPENZI
Wakati mwingine watu hushindwa kuwaamini wenzao, lakini kwa sababu ambazo ni za msingi, lakini kuna wakati ambapo mtu hushindwa kumwamini mwenzake bila sababu yoyote ya msingi, au kwa sababu zisizo sahihi, kisingizio kikiwa ni mapenzi.

Kuna tatizo la kisaikolojia la kujishuku au kuwashuku wenzako. Hili ni jambo ambalo linaweza kukuharibia mustakabali wako katika mapenzi, maana husababisha kujengeka kwa mazingira ya kutokuaminiana. Ili uweze kwenda sanjari na mpenzi wako, amini kila anachokweleza hadi pale utakapokuwa na sababu za msingi za kutokumwamini. Na hata unapokuwa umelithibitisha jambo, endelea kuwa katika uhalisia wako.

6. KUACHA HOBI, MARAFIKI
Mahusiano ya kimapenzi mara nyingi huhusisha kila mmoja kuacha baadhi ya mambo yake kwa ajili ya mwenzake. Hata hivyo, lengo ni kuweka tu uwiano wa mahitaji, si kuacha kila kitu ulichokuwa nacho kwa ajili ya mwenzako, ama kwa shinikizo, au kwa kulewa penzi.

Iwapo utabaini kuwa marafiki zako sasa wamekuwa ni marafiki zako wa zamani na hobi zako zimebaki tu katika kumbukumbu japo kwa hakika bado unahisi mapenzi katika hobi hizo, basi tambua kuwa huyo mrembo wako amekunywesha sumu ya penzi na sasa huwezi hata kuitumia vema mantiki yako.

Mbaya zaidi, iwapo utabaini kuwa marafiki zako wapya ni marafiki wa siku zote wa mpenzi wako na hobi zako ni zile za mpenzi wako, basi tambua kuwa huna tena nafsi yako, bali umejisalimisha mzima mzima kwa mpenzi wako. Lakini msemo mmoja wa hekima unatwambia usiweke mayai yako yote kwenye kikapu kimoja. Yamkini unaelewa.

7. KUKUBALI KUPELEKESHWA
Pengine unakumbuka kuwa kuna nyakati ambapo ulikuwa na uwezo wa kujikita katika jambo moja na kulifanya kwa umakini, huku ukiwa pia mwerevu, mjanja na unayejisimamia, lakini leo unayeyuka kirahisi tu kama barafu iliyowekwa juani! Hii ni hatari kwa mustakabali wa maisha yako.

Mbaya zaidi ni pale utakapoiacha kazi yako inayokulipa vizuri na kufanya kazi nyingine kwa ajili ya kumfurahisha mpenzi wako. Ukifika hali hii ujue wewe mwenyewe kuwa hapo hakuna mwanamume.

8. UTAYARI WA KUFA KWA AJILI YAKE
Umewahi kujisikia kuwa na utayari wa kufa kwa ajili ya mpenzi wako? Kama jibu ni “ndiyo”, basi fahamu kwa hakika kuwa hayo uliyo nayo si mapenzi bali ni upumbavu. Pengine huku ndiko kunywesha sumu ya mapenzi. Kwa hakika, hakuna mwanamke ambaye anastahili kumfanya mwanamume yeyote kufa kwa ajili yake.

Yamkini wanaume wanaolengwa katika makala haya si wavulana wanaosoma sekondari, waliobalehe majuzi, ambao wakipenda au kupendwa hujiona kama wako katika sayari yao. Mwanamume aliyepevuka hujiamini na hayaweki maisha yake yote mikononi mwa mwanamke, hata kama mwanamke huyo angekuwa ndiye mrembo wa dunia.

Iwapo, ama kwa ujinga au kwa kufahamu umewahi kumwambia mpenzi wako: “Ukiniacha nitajiua,” na ukawa unaamini hivyo kabisa, basi yamkini unahitaji kutafuta msaada wa ushauri nasaha, maana kwa hakika umepotoka.

9. MUDA WOTE UNAWASILIANA NAYE
Vijana wa siku hizi ni watumiaji wazuri sana wa simu, lakini iwapo utabaini kuwa asilimia kubwa ya muda wako unautumia ama kwa kuongea au kuwasiliana kwa ujumbe mfupi na mpenzi wako, basi fahamu kuwa kuna tatizo ambalo linahitaji ufumbuzi wa haraka.

Kumbuka kuwa mapenzi hayachukui nafasi ya kila kitu. Yamkini huyo mpenzi wako amekukuta unaishi na kuna mambo ya muhimu ya kufanya. Hebu achana na simu kwanza ufanye mambo ya muhimu kuhusiana na maisha yako. Kama mpenzi wako hakwelewi katika hili basi hakufai.

10. NDUGU ZAKE WANAKUFUATILIA
Iwapo utabaini kuwa marafiki, ndugu na jamaa za mpenzi wako wanamtonya mpenzi wako kuhusiana na kile wanachokiita mwenendo wako mbaya, usipuuze hali hii. Kuna uwezekano mkubwa kuwa watu hawa wanayo sababu ya kuwa na wasiwasi na mwenendo wako, kwa hiyo jichunguze na kuangalia jinsi unavyoenenda.

Hata hivyo, jambo hili si ishara njema ya mustakabali mwema wa uhusiano wenu. Iwapo mpenzi wako ataweka watu wake wakufuatilie, maana yake halisi ni kwamba hakuamini. Katika hali kama hii, haitarajiwi kuwa mustakabali wa uhusiano wenu utakuwa mzuri, kwani kutakuwa na uingilizi mwingi wa ndugu, jamaa na marafiki zake. Unaweza kukubali kuendelea kuishi katika hali hii kwa kisingizio cha mapenzi, lakini ukweli ni kwamba hayatakuwa mapenzi bali karaha.

KUWA MAKINI
Kama unavyoona, hizi ni baadhi tu ya dalili kuwa mapenzi yako kwa mwanamke sasa yanaelekea katika ulevi, mithili ya ule wa dawa za kulevya. Jambo moja la kukumbuka ni kwamba kweli mapenzi ni kitu kizuri, lakini pia mapenzi yanahitaji kuwa jambo linaloashiria mustakabali mwema kwa wahusika wawili. Yakiwapo mambo haya kumi hauwezi kuwapo mustakabali mwema katika mapenzi.

KAMA HAWA WAMEWEZA JE WEWE UNASHINDWA NINI??

KAMA HAWA WAMEWEZA JE WEWE UNASHINDWA NINI KAMGISHA BLOG / 9 hours ago

SUMU YA MAFANIKIO NI KUKATA TAMAA AU KUOGOPA CHANGAMOTO, EMBU TAZAMA PICHA HIZI UTAWEZA KUJIFUNZA KITU NDANI YAKE..




















Mbao Fc yachezea kichapo cha magoli

Mbao Fc yachezea kichapo cha magoli 21

KAMGISHABLOG / 3 hours ago

Timu ya Mbao FC ya Dodoma imekubali kichapo cha mbwa mwizi baada ya kufungwa mabao 21 dhidi ya timu ya Panama FC kwenye mchezo wa Kombe la Ng’ombe mjini Dodoma.

Kichekesho zaidi kama sio rekodi ni mshambuliaji wa Panama FC, Dulla Mjengwa aliibuka kinara wa mabao 13 lakini hakuambulia zawadi ya mpira wowote kama inavyotakiwa.

Mechi hiyo ilipigwa jana Jumamosi kwenye Uwanja wa Mtekelezo uliopo katikati ya mji, ambapo ilishuhudiwa timu hiyo ya Mbao ikitokota tangu mwanzo mbele ya Panama kwani hadi mapumziko ilikuwa imeshakula bao 10 na kuruhusu bao zingine 11 kipindi cha pili.

Mratibu wa ligi hiyo, Rashid Nyoka baada ya kuulizwa sababu za kutotoa zawadi ya mpira kwa mfungaji huo alisema, walishindwa kumpatia mpira mfungaji huyo kutokana na ligi hiyo kutokuwa kanuni zao kutoweka kipengele cha zawadi hiyo.

Kipigo hicho kiliwafanya viongozi wa timu hiyo ya Mbao wasizungumze lolote ambapo wengine walidai timu hiyo ilikata tamaa kutokana na kufungwa mechi zilizopita na kukosa nafasi ya kutinga robo fainali huku wengine wakiwashtumu viongozi wao kuwa walipanga kikosi dhaifu.

Mzee cheyo awavaa sumaye na lowassa

Mzee Cheyo awavaa Sumaye naLowas KAMGISHA BLOG / 2 hours ago

Mwenyekiti wa Chama cha United Democratic (UDP), John Momose Cheyo maarufu kama `Bwana Mapesa’ amesema jukumu la viongozi wastaafu ni kuwaweka pamoja watanzania na siyo kuwafarakanisha kwa tofauti za kisiasa, kidini na uchama.

Akizungumza juzi jijini Dar es Salaam wakati akitambulisha ofisi za chama hicho zilizohamia Mwananyamala A, Cheyo amesema anashangazwa na mawaziri wakuu wastaafu ambao walihamia upinzani na kuanza kutoa kauli ambazo kwa namna moja au nyingine zinaharatarisha amani.

“Upinzani sio kupinga kila jambo, wastaafu jukumu lao ni kufanya mambo ya kutuweka pamoja na sio kutufarakanisha,” amesema Cheyo.

Mh Cheyo amesema kuingiza mambo ya dini katika siasa ni kutafuta mfarakano baina ya  wananchi na kwamba kwa maoni yake kiongozi ambaye ameshika nafasi kubwa kama Waziri Mkuu hatarajiwi kuliingiza taifa katika mafarakano.

“Maendeleo hayana vyama, Rais tuliye naye anafanya mambo na yanaonekana tumuunge mkono tuachane na itikadi za vyama, au wanataka tusubiri mpaka chama fulani kiingie madarakani ndipo tupate maendeleo?” alihoji Mh Cheyo.

Hata hivyo Mh Cheyo amepongeza jitihada mbalimbali zinazofanywa na Rais wa awamu ya tano, Mh Dkt. John Magufuli na kuijenga Serikali imara, yenye kulinda maslahi ya nchi na ustawi wa watu wake.

Hivi karibuni, Waziri Mkuu wa mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa aliitaka Serikali kuwaachia huru mashehe wa Uamsho wanaoshikiliwa kwa zaidi ya miaka minne sasa.