Tafuta katika Blogu Hii

Jumatano, 30 Mei 2018

*JE IMANI AU MAPOKEO YA KANISA KATOLIKI YANAPATIKANA KATIKA BIBLIA?*

*JE IMANI AU MAPOKEO YA KANISA KATOLIKI YANAPATIKANA KATIKA BIBLIA?*
*&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&*

Wakatoliki wengi huyumbishwa kwa kuambiwa huamini mambo ambayo hayako au ni kinyume na Biblia. Aya zifuatazo zitakusaidia wewe mkatoliki kuelewa au kujua mistari ya Biblia inayofafanua  imani katoliki.

1) KUOMBEA MAREHEMU:
     2 Mak. 12:38-46
      Hek. 3:1
      Tob 4:17

2) MATUMIZI YA SANAMU NA VISAKRAMENTI
     2Fal 3:20-21
      Hes. 21:8-9
      Kut. 25:17-22
      Kol. 1:20, 2:14
      Yn. 12:32
      Mt. 19:11-12

3) USAHIHI WA MAPOKEO YA KANISA KATOLIKI KAMA CHANZO CHA IMANI
        2 The 2:15
        2 Kor. 10:10-11
         Yn 21-25
         2 Yoh. 1:12
         3 Yoh. 1:13

4) KUABUDU JUMAPILI BADALA YA JUMAMOSI(SABATO).... Hasa ni kwa sababu Yesu aliitukuza siku ya kwanza ya juma kwa ufufuko wake na kwa kuwatokea wanafunzi wake siku hiyo.
         Ufu 1:10
         Mdo 20:7
         Mt 28:1-8
         Lk. 24:1-7
         Lk. 24:13ff
         1 Kor. 16:1-2
         Yn. 20:1-22

5) MAMLAKA YA PAPA KAMA MFUASI AU MRITHI WA MT. PETRO
         Yn. 21:15-17
         Mt 16:18-19
         W 2:1-14
      
6) MAPADRI KUITWA BABA WAKATI BABA NI MMOJA ALIYEKO MBINGUNI
          Mwa 17:4
          Yer. 7:7
           Hes. 12:14
           Yn. 6:49
           Mt 23:30
           Lk. 1:73

7) JE BIBLIA INATAMBUA MUUNDO WA UONGOZI WA KANISA?
          Efe. 4:11-13
          1Tim 5:17-25
          1Tim 3:1-7,8-18

8) JE BIBLIA INASEMAJE KUHUSU TOHARANI.
           Isa 35:8, 52:1
           Zek 13:1-2
           1Kor 3:15
            Lk 12:47-48, 58-59
           Ufu 21:27
           Ebr 12:22-23
           Ayu 14:13-17

9) KUHUSU MATUMIZI YA UBANI
          Kut 30:34-37
          Hes 16:6-7
          Law 16:12-13
          Lk 1:10
          Ufu 8:3

10) ROZARI IKO KATIKA BIBLIA?
           Lk 1:28
           Lk 1:42
   
11) JE KUTUMIA MAJI YA BARAKA NI MAPENZI YA MUNGU?
           2Fal 2:19-22
           Yn 5:1-18
           Yn 7:37
            Hes 19:1-22

12) KWANINI TUNAOMBA WATAKATIFU WATUOMBEE?
           Mit  15:8, 15:29
           Ayu 42:8
           Yak  5:16
            Mt 16:19

13)KWANINI TUNATUMIA MEDALI, MISALABA, SCAPURALI NA MIFUPA YA WATAKATIFU?
           2Fal 13:20-21

14) KWANINI TUNAUNGAMA DHAMBI ZETU KWA PADRI
         Mt 16:19,1-20
         Yak 5:15-16

15) UBATIZO WA WATOTO WACHANGA UKO KATIKA BIBLIA
           Mdo 16:15-33
           Mdo 18:8
           Mt 28:19
           Mdo 10:47-48

16) KUSIMIKWA KWA UTUME
          Kut 28:4-43

17) RANGI ZA KANISA
         Kut 27:9-29

18) MATUMIZI YA MISHUMAA
       Kut 25:31-40; 27:20-21
       Hes 8:1-4

19) MPAKO WA MAFUTA YA KRISMA
      Kut 30:22-32

20) MPAKO WA MAFUTA YA WAGONJWA
       Yak 5:14-15
*Hii ni kwa ajili ya wakatoliki wote wasiokua na uhakika wa wao kuwa wakatoliki*
*~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~*
Mtumie na mkatoliki mwenzio ili tujijenge kiimani na kiroho pia.
   
       *Roho wa Bwana awe nawe*

Jumapili, 29 Aprili 2018

Methali

​​​Kuna Methali zimekwisha muda wake wa matumizi.
Mfano:​​​
1. Mwenzako akinyolewa tia maji.
_*• Siku hizi tunanyoa kwa mashine.
Ukitia maji zinateleza hazinyoleki.
Mara wapgwa shot ya umeme uvurugike akili *_

2. Barua ni nusu ya kuonana.
_*• Siku hizi watu wanaonana kwa watsap.
Mkingojea barua mtakufa bila kuonana.*_

3. Akili ni nywele.
• Vipi kuhusu Mawigi?

4. Mchagua jembe si mkulima.
• siku hizi tunatumia zaidi matrekta ya kukodi.

5. Alalae usimuamshe akiamka utalala wewe.
• siku hizi unaweka alam mwenyewe unaamka hausubiri kuamshwa na mtu.

6. Polepole ndio mwendo.
• siku hizi kuna mwendo kasi ukienda polepole utabaki kwenye foleni kutwa

Hatupendi mambo ya kizamani...

Uwe na asubh njema..nakwenda kulala kidooogo prt 2

Jumapili, 15 Aprili 2018

Ulishajiuliza Unapenda Nini Kwa Mpenzi Wako ?

Ulishajiuliza Unapenda Nini Kwa Mpenzi Wako ?


Kamgisha blog.Darasa la Mapenzi / 3 days ago



Leo kwenye safu hii nimekuja tuongelee suala hili la wapenzi kupendana na kufikia kuwa mwili mmoja je, umewahi kujiuliza maswali kuhusiana na mwenza wako? Maswali haya yanawahusu wote.

Mnatafuta nini ndani ya wenza wenu ni kitu gani mnaangalia/mnakiona ndani ya mtu unayeamua kuwa naye kama mchumba/mume/mke. Je, ni macho yake au tabasamu, ama ni muonekano wake, uchangamfu au upole, ni kitu gani unachokiona ndani ya mtu kinachokuvutia. Wengine wanavutiwa jinsi mtu anavyofikiria, au mwili wake, wewe je?

Unaweza ukawa umevutiwa na kitu kimojawapo, lakini unajua uhusiano mzuri haujengwi na vitu hivi tu, kuwa na uhusiano mzuri na mwenza wako inahusisha vitu vingi sana tofauti na tabasamu lake iwe unatafuta mtu wa kuwa naye au kama tayari upo katika uhusiano hakikisha mnakubaliana vitu muhimu ambavyo mkividharau kisa umempenda kwa sababu ya shepu yake au ucheshi wake vinaweza kuharibu uhusiano huko mbele ambapo ni pagumu zaidi.

Vitu unavyotakiwa kuangalia zaidi

Hivi ni baadhi ya vitu unavyotakiwa kuangalia ndani ya mwenza wako kama unataka uhusiano mzuri na kama kweli atakuwa mke au mume, epuka kuangalia vitu vya awali kama hivyo nilivyovitaja hapo.

Anakupa heshima yako, haijalishi kama yeye ni mkubwa kwako, na hapa heshima siyo salamu kama wengi mnavyodhani.

Anaheshimu maamuzi yako, kama ni katika kazi au kitu unachoamua kufanya na siyo kukucheka au kukudharau.

Hakukatishi tamaa anakuunga mkono kwenye kila jambo na kukupa moyo wa kushinda kila wakati.
Hakasiriki ukijipa muda na marafiki au familia yako, unatakiwa kuwa na uhuru wa kujichanganya na watu wengine siyo yeye tu.

Anasikiliza mawazo yako na kukushauri

Mnashea vitu unavyovipenda kama vile kuangalia muvi, aina ya muziki, kucheza. Angalau muwe na kitu kimoja ambacho wote mnapenda ili muwe na kitu cha kufanya pamoja, vitu vingine mnaweza kutofa-utiana haina shida kwa sababu hata mapacha waliozaliwa pamoja kuna wakati huwa wanato-fautiana lakini iwe kuna kitu mnaendana ambacho mtashiriki pamoja.

Mpenzi huyo asiwe mkaidi kwa kila kitu unachomwambia, hii inawahusu wapenzi wote si wanaume ama wanawake tu.

Awe anaheshimu mipaka yako, siyo atake kujua kila kitu chako kama vile kukagua simu au wapi unapokuwa saa 24, kama mpo katika uhusiano mnatakiwa mheshimiane maana mwanzo wa kufuatiliana saa zote ndiyo mwanzo wa ugomvi usiyoisha.

Asiogope kukuambia anavyojihisi, hii itawasaidia hata pale mtakapokuwa na matatizo ili muweze kusuluhisha mambo yenu, itawaondoa kwenye hali ya kila mtu kumuwekea mwenzake kinyongo.

Kumbuka uhusiano unahusisha watu wawili, wewe na patna wako muwe na usemi ndani ya uhusiano wenu na msiogope kuambiana mnachohisi na kusikilizana pia.

Ndani ya kila uhusiano kuna kugombana, hiki ni kitu cha kawaida kabisa. Wale mnaowaona wana furaha katika uhusiano wao wameweza kujua jinsi ya kuyamaliza matatizo yao.

Usimpende mtu kwa sura, fedha, uvaaji wake bali iwe kwa mapenzi ya dhati.

Ijumaa, 2 Machi 2018

ASIKUCHOSHE NA MANENO YAKE YA SHOMBO ANGEKUA NA UWEZO WA HAO WAZURI ASINGEKUFUATA WEWE!

ASIKUCHOSHE NA MANENO YAKE YA SHOMBO ANGEKUA NA UWEZO WA HAO WAZURI ASINGEKUFUATA WEWE!

Akikuambia sijui kwanini nilioa mwanamke kama wewe tabasamu na muambie ni kwakua hukua na uwezo wa kupata mwingine bora zaidi yangu hivyo si kwamba wewe umenizidi chochote bali nikwakua tunaendana! Hata kama huna ujasiri wa kumuambia hivyo lakini jiambie wewe mwenyewe, jiambie ukijua kua kama angekua ni bora kuliko wewe kama anavyojinadi kila mara basi angeoa hao anaowaona kama ni bora kuliko wewe.

Ukiona mwanaume kila mara mnapogombana maneno yake ndiyo hayo basi jua kuwa tatizo si wewe bali tatizo ni yeye, hajiamini ndiyo maana analazimika kukushusha ili ahisi kama vile mko sawa. Acha kushuka na kuwa kama yeye, acha kuumia na kujiona kama takataka mbele yake kwani ukweli nikua mpaka anakuja kukutongoza au mpaka anakubali kuwa na wewe basi alikupenda au wewe ni wa aina yake. Kama usingekua wa aina yake usingemvutia na asingekufuata!

Asikuchoshe na maneno yake ya shombo kwani kama angekua na uwezo wa hao anaowaona ni wazuri mbona angewafuata wao lakini hakua nao na akabaki na wewe! Mwisho kumbuka kuwa jinsi ulivyo ndivyo ambavyo Mungu alitaka uwe hivyo, angetaka kukuumba kivingine angefanya hivyo na alikua na uwezo huo lakini hapana, aliamua uwe hivyo na huna sababu ya kujichukia na kujiona takataka kisa tu una mwanaume ambaye hajiamini!

Alhamisi, 8 Februari 2018

Umuhimu wa Kujiongeza katika maisha ya mafanikio


Muungwana Blog · 12 hours ago




Habari za muda huu mpenzi msomaji wa mtandao huu wa dira ya mafanikio, ni matumaini yetu mazima u mzima wa afya tele na unaendelea vyema katika harakati zako za kuweza kulisukuma gurudumu hili la maendeleo.  Ni siku nyingine tulivu ambayo sina budi nikukaribishe kwa moyo mkunjufu tuweze kujifunza kwa pamoja. 

Siku ya leo nataka ttuzungumzie namna ambayo una uwezo mwingine wa kutenda jamno jingine ambalo linaweza kukupa mafanikio makubwa kwa upande wako tofati na hilo ulitendalo sasa. Unajua nataka tuzungumzie hili kwa sababu wetu wengi hawafahamu uwezo mwingine walionao, ambao unaweza kuutumia ili uweze kukamilisha jambo jingine ambalo Mwenyezi mungu kakujalia kiulitenda. 

Watu wengi hudhani ya kwamba hicho ambacho wanakifanya ndicho ambacho wamepangiwa kufanya. Kwa mfano mtu ni mfanyabishara fulani, labda huenda mtu akawa amesomea kitu fulani, basi baada kuweza kubobea katika kipengekle hicho, basi anaweka mipaka katika kitu hicho pekee. 

Ukweli haipo hivyo hata chembe, kwani kila binadamu binadamu kaumbwa  na uwezo mwingine wa kufanya vitu vingi ambavyo vitaweza kumuinua kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine ya kimafanikio. Hata kanuni ya kufanya mazoezi ya mwili inasema ya kwamba huwezi kutengeneza six park kwa kufanya mazoezi ya aina moja pekee kila wakati, bali unaweza kutengeza six park kwa kufanya mazoezi ya aina tofauti tofauti. 

Kwa  muktadha huo kama kweli unataka kufanikiwa zaidi ya hapo ulipo sasa, unachotakiwa kufanya ni kuweza kutambua uwezo mwingine ambao mwenyezi Mungu kakuwekea ndani yako, ili uweze kujipatia mkate wako wa kila siku. 

Hata mwandishi mmoja aitwaye Antony Robbison aliwahi kuandika ya kwamba “if you do what you have done you will get what you always gotten” hii ikiwa na maana “kama utafanya mambo yaleyale ambayo umekuwa  ukifanya siku zote, utapata yale yele ambayo siku zote umeyapata”. Naomba urudie kusoma tena aya hii ili uielewe vizuri. 

Kwani aya hiyo ipo wazi kabisa kama umezoea kufanya mambo yale yale kwa njia ile ile basi matokeo yake, yatakuwa ni yaleyale. Hivyo ili uweze kupata matokeo ya iana tofauti  na uliyoyazoea, unachotakiwa kufanya kubomoa uzio wako wa kufikiri kwa kuanza kubadili ratiba ya kutenda mambo yako ya msingi. Lakini pia ongeza uzio wa kufanya mambo yako  kwani binafsi naamini una kitu kingine cha kufanya zaidi ya hicho ambacho unakifanya. 

Mwisho nimalizie makala haya kwa kusema ukitaka kwenda mbali zaidi katika mambo yako ya msingi acha kujenga uzio ambao utakufanya ushindwe kuona fursa nyingine,  bali unachotakiwa kufanya ni kubomoa uzio huo ili uweze kuona fursa mbalimbali ambazo zimejificha, kwani pindi unavyoacha ukuta huo ni kule kutengeneza uwezo wako wa kulalamika, na mwisho wa siku kuelekea jehenamu ya umasikini. 

Narudia kwa kusema tena pale unaposhindwa kujiongeza ni kutengeneza jehanamu ya umaskini. Usiogope na kusema afisa mipango anakutisha hapana,  ila kazi yangu ni  kukwambia ukweli ambao upo wazi, kwani nafasi uliyonayo sasa unachotakiwa kufanya ni kuwaza ni namna gani utaweza kufika mbali zaidi. 

Kwani umuhimu wa kujiongeza kunamsaidia mtu kuweza kuwa milango mingi ya kuweza kufanikiwa zaidi. Pia faida nyingine ya kujiongeza humsaidia mtu kuweza mbunifu zaidi kwa kile akifanyacho. Na ubunifu humsaidia mtu aweze kujilikana na ukijulikana ndo mwanzo wa mafaniko yenyewe. Mpaka kufikia hapo sina la ziada naomba kazi ibaki kuwa kwako kwa kuamua kwenda kuyatekeleza hayo ambayo nimekwambia. Asante.Ni wako katika ujenzi wa mafaniko. 

Jumatatu, 15 Januari 2018

Sababu

Sababu kuu 7 za kwanini kila mwanaume anahitaji mwanamke sahihi

Muungwana Blog 5 · Yesterday



Kwangu kipindi ambacho kilinivutia sana ni kipindi cha kampeni za uchaguzi nchini Marekani. 

Ni pale Obama akiwa katika kampeni kwenye moja ya majimbo kugombea duru ya pili ya uraisi aliposimamisha hotuba yake na kutambua uwepo wa mkewe Michelle. 

Obama alisema, "Mke wangu amekuwa bega kwa bega na mimi tokea niko chuo, kuna kipindi nilishindwa kulipa ada ila yeye ndiye aliyenilipia" 

Obama akaenda mbali zaidi na kukiri mbele ya jamii ya kimataifa kwamba asingekuwepo hapo alipo kama sio mke wake Michelle. 

Hivyo basi, nashauri kwamba mwanamke ambae mwanaume atakua nae huenda akawa chachu ya mafanikio na baraka kwake au anaweza akamrudisha nyuma kabisa katika mipango yake. 

Sababu kuu 7 za kwanini iwe isiwe mwanaume lazima upate mwanamke alie sahihi. 

1. Kila mwanamke anao uwezo wa kukuridhisha kimapenzi ila mwanamke sahihi na bora pekee ndiue anaeweza kuku-challenge kiakili na kuwa 'intellectually inspired'. 

2. Mwanamke yeyote anaweza kukuteka kihisia, ila yule sahihi pekee ndiye mwenye uwezo wa kukuteka kiroho na ukamtumikia Mungu wako. 

3. Mwanamke yeyote anaweza akakushawishi muandike mpango wa harusi (wedding plan), ila mwanamke sahihi peke yake ndie mwenye uwezo wa kukuandikia na kukushauri mpango wa biashara (business plan) 

4. Kila mwanamke anaweza akakubusu tena 'French kiss' ila mwanamke bora pekee ndio mwenye uwezo wa kukutamkia maneno yaliyojaa busara na hekima. 

5. Kila mwanamke anaweza akakupenda sana tu tena kama una pesa, ila mwanamke aliye bora pekee ndiye anaeweza kusimama na wewe hata kukuinua pale utakapokuwa huna kitu. 

6. Mwanamke yeyote anao uwezo wa kukushibisha kwa kukupikia chakula kitamu, ila mwanamke bora pekee ndio mwenye uwezo wa kukulisha chakula cha ubongo. 

7. Kila mwanamke anao uwezo wa kukushawishi chumbani ila mwanamke bora pekee ndio mwenye uwezo wa kukushawishi umrudie Mungu wako. 

Mwisho ngoja nihitimishe kwa kusema hivi ukisoma vitabu vya kihistoria kuhusu Winstom Churchhill mpaka Abraham Lincoln, na kutoka kwa Nelson Mandela mpaka kwa Martin Luther King Jr lao moja kwamba “No matter how strong a Man is, he is only as strong as the Woman he marries” Kwa tafsiri yangu ya kuunga unga isiyo sahihi sana Wanamaanisha "haijalishi ni kwa kiasi gani mwanaume una nguvu, nguvu zako zina athiriwa kwa kiasi kikubwa na mwanamke utakaemuoa"

Jumatatu, 8 Januari 2018

King mafla misemo ya ukweli

M


MandagoJF-Expert Member

#1Oct 5, 2010Joined: Feb 8, 2008Messages: 238 Likes Received: 80 Trophy Points: 45

Baadhi za Hekima na Methali za Kiarabu

1) Si vigumu kujitolea kwa kumsaidia rafiki yako,lakini ni vigumu kupata rafiki ajitolee kwa ajili yako.

2) Usiache ulimi wako ukafuata macho yako kwa kueleza aibu za watu, kumbuka kuwa watu nao wana macho na ulimi kama wewe.

3) Mambo yasiyokuwa na umuhimu huzungumzwa kwa muda mrefu kwani sote tuna yafahamu kuliko mambo muhimu.

4) Ikiwa una mikate miwili kula mmoja na mwingine utowe sadaka.

5) Mtu akisifiwa watu wachache huamini,lakini akikashifiwa wengi huamini.

6) Hakuna mtu ambaye hakufanikiwa kabisa,bali ameanzia na sifuri akabakia hapohapo. 

7) Binaadamu ambaye amefaulu ni yule anaye nyamaza kabla ya watu hawaja ziba masikio yao, na anafunguwa masikio yake kabla ya watu hawajafunguwa midomo yao. 

8) Kabla ya kuzungumza chaguwa neno la kusema, na uchukuwe muda wa kusema ili maneno yako yachipuwe kama linavyo chipuwa tunda.

9) Jihadhari na mtu ambaye ni mkarimu ukimdharau,na mtu mbaya ukimkarimu,na mwenye akili ukimkosowa na mjinga ukimrehemu.

10) Ukifikia kilele mwangalie jambazi ili upate mtu wa kukusaidia,na angalia mbinguni ili Mwenyeezi Mungu akuweke imara usianguke. 

11) Si kufaulu kugunduwa mambo wanayo yapenda watu,lakini kufaulu ni kuwa na ujuzi wa kuwafanya watu wakakupenda.

12) Shujaa anaye jitahidi kutatuwa matatizo yake,anafaidika na uwezo wake

13) Ukipanda jabali angalia kilele chake,wala usiangalie upande wowote na ulipande kwa makini,wala usiruke ukavunja mguu wako.

14) Shujaa ni yule ambaye anauwezo wa kukuza ujuzi wake,na kuweza kukuza ujuzi wa watu na pengine kuwabadilisha.

15) Usiache utajiri ukakufanya ukakosana na watu,kwani kuwa pamoja na watu ndio njia ya kuupata utajiri.

16) Badali ya kukaa na kutukana kiza,jaribu kutengeneza umeme. 

17) Ukitabasamu tabasamu kwa mtu masikini, kwani kunakuongezea malipo mema kwa Mwenyeezi Mungu.

18) Mwanamke humsubiria mume wake kwa umasikini wake,ubaya wake na kutokumjali kwake ,lakini hamsubirii kwa tabia mbaya yake.

19) Mtoto ni kama udongo(wa ufinyanzi) tuna mlea kwa jinsi tunavyo ona sisi. 

20) Watendee watu kama wao ni binaadamu si kwa sura zao wala pesa zao wala vyeo vyao. 

21) Uzuri wa mtu ni ndani ya nafsi yake,si sura yake. 

22) Ukisema neno litakumiliki,na usipolisema utalimiliki.

23) Anaye ishi na sura mbili,hufa bila ya sura

24) Adui yako akikuomba ushauri mpe nasiha,kwani ukimpa ushauri ataondosha uadui wake kwako na kukusaidia.

25) Ukizungumza wakati ukiwa na hasira,utasema neno ambalo utajutia maisha yako.

26) Usijadiliane na mtu mjeuri wala asiyekuwa na haya, kwani jeuri hutomuweza na asiye na haya atakuudhi.

27) Tabia njema ina sitiri mambo mengi mabaya,na tabia mbaya ina ziba mambo mengi mazuri.

28) Mwenye kumuamini Mwenyeezi Mungu humpa,mwenye kutawakal kwake humtosha,mwenye kumuogopa huacha aliyo yakataza na mwenye kumjuwa humuenzi.

29) Kunyamaza ni dalili ya kukubali jambo.

30) Jihadhari na ulimi wako,usiiponze shingo yako. 

31) Fimbo ya muongo ni fupi.

32) Si kila wakati mtu husalimika na jirani.

33) Ulimi wako ni kama farasi wako,ukiuchunga vizuri nao utakuchunga na ukiuachia nao utakuponza.

34) Ndege mmoja aliye mkononi mwako ni bora,kuliko kumi waliyoko katika mti.

35) Kila kimya kina jambo lake.

36) Ukitaka kutiiwa,amrisha mambo yanayo weza kufanywa.

37) Wezi wawili wakigo mbana ,vitajulikana vitu vilivyo ibwa.

38) Jihadhari na shari hata kwa mtu uliye mfanyia mema.

39) Upanga umeshinda kanuni.

40) Mwanzo wa mavuno ni tone la mvuwa.

41) Kuwa na haya ni katika imani.

42) Mazungumzo mazuri huwa mafupi na yanayo eleweka.

43) Mwaka ni kama siku mbili,siku kupata na siku kukosa.

44) Huto pata hasara ukimshauri mtu.

45) Haraka hutokana na shetani.

46) Kila kiongozi,na hotuba yake.

47) Mwenye kuingilia jambo lisilo muhusu,husikia yasiyo mridhisha.

48) Wakati ni kama upanga usipo ukata utakukata.

49) Haurushiwi mawe,isipokuwa mti wenye matunda.

50) Mwenye kuwachunguza watu hufa kwa kiroro(hamu). 

51) Watu bora zaidi ni wale wanao towa daawa kwa vitendo vyao kabla ya maneno yao.

52) Uwezo wa kuathiri nyoya za watu,na kupata pendo lao la kweli hutuletea furaha kubwa katika maisha yetu.

53) Nia nzuri ni kufanya ujuzi wa kuwafanyia watu mambo ya ibada,kwani hukukurubisha na Mwenyeezi Mungu(huwa karibu na Mweyeezi Mungu) 

54) Usifikirie watu wote ni sawa,kwani kuna watu wenye tabia tofauti kuliko aina za rangi

55) Zungumza na watu kwa mambo ambayo wana penda kuyasikia,siyo kwa mambo ambayo unaya penda wewe.

56) Mkutano wa kwanza huchukuwa asilimia thamanini ya tabia ya mtu anavyo onekana, wafanyie watu wote kama kwamba huo ni mkutano wa kwanza na wa mwisho kati yenu.

57) Kuijuwa tabia ya mtu ndio kuna kupa uwezo wa kupata pendo lake.

58) Kila mtu ana ufunguo wake,kwa kujuwa tabia ya mtu ndio kujuwa njia ya kuelewana nae.

59) Binaadamu hufanya mambo yote kwa moyo wake siyo kwa mwili wake.

60) Ukimiliki nyoyo za watu hupendeka

61) Mtu kujitahidi kutoingilia mambo yasiyo muhusu ni vigumu lakini humpumzisha.

62) Kuwa kama nyuki anatuwa juu ya kitu kizuri na kujiepusha na kitu kibaya, usiwe kama inzi kutuwa juu ya vidonda.

63) Huwezi kula asali bila ya kuvunja nyumba ya nyuki.

64) tukifanya watu wajuwe kwamba tunaangalia mazuri yao kabla ya mabaya yao watakubali kupokea nasiha.

65) Ni bora mtu kujuwa kosa lake si sharti kulisahihisha mbele ya watu.


R

ReasoningMember

#2Oct 6, 2010Joined: Mar 7, 2009Messages: 57 Likes Received: 0 Trophy Points: 0

Asante Mandago. Hakika ni misemo iliyojaa hekima sana. Chukua tano!!!


myao wa tunduruJF-Expert Member

#3Oct 6, 2010Joined: Mar 9, 2010Messages: 613 Likes Received: 20 Trophy Points: 0

ubarikiwe mkuu Mandago....nimejifunza kitu


MahmoodJF-Expert Member

#4Oct 7, 2010Joined: Feb 9, 2008Messages: 7,851 Likes Received: 1,336 Trophy Points: 280

Asante sana ndugu Mandago kwa haya maneno yenye hekima kubwa, nimejifunza mengi katika meneno haya ya hekima.


(You must log in or sign up to reply here.)

 Facebook


 Twitter


 LinkedIn


 Google+


 Pinterest


 Email


WHO ARE WE?


JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic. You are always welcome!

Read more...


WHERE ARE WE?


We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually. For anything related to this site please Contact us.

Contact Us Now...


DISCLAIMER


JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

Read more...


FORUM RULES


JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you. You MUST read them and comply accordingly

Read more...


PRIVACY POLICY


We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one. Read our Privacy Policy.

Proceed here...



Contact Us


Help