Tafuta katika Blogu Hii

Alhamisi, 8 Februari 2018

Umuhimu wa Kujiongeza katika maisha ya mafanikio


Muungwana Blog · 12 hours ago




Habari za muda huu mpenzi msomaji wa mtandao huu wa dira ya mafanikio, ni matumaini yetu mazima u mzima wa afya tele na unaendelea vyema katika harakati zako za kuweza kulisukuma gurudumu hili la maendeleo.  Ni siku nyingine tulivu ambayo sina budi nikukaribishe kwa moyo mkunjufu tuweze kujifunza kwa pamoja. 

Siku ya leo nataka ttuzungumzie namna ambayo una uwezo mwingine wa kutenda jamno jingine ambalo linaweza kukupa mafanikio makubwa kwa upande wako tofati na hilo ulitendalo sasa. Unajua nataka tuzungumzie hili kwa sababu wetu wengi hawafahamu uwezo mwingine walionao, ambao unaweza kuutumia ili uweze kukamilisha jambo jingine ambalo Mwenyezi mungu kakujalia kiulitenda. 

Watu wengi hudhani ya kwamba hicho ambacho wanakifanya ndicho ambacho wamepangiwa kufanya. Kwa mfano mtu ni mfanyabishara fulani, labda huenda mtu akawa amesomea kitu fulani, basi baada kuweza kubobea katika kipengekle hicho, basi anaweka mipaka katika kitu hicho pekee. 

Ukweli haipo hivyo hata chembe, kwani kila binadamu binadamu kaumbwa  na uwezo mwingine wa kufanya vitu vingi ambavyo vitaweza kumuinua kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine ya kimafanikio. Hata kanuni ya kufanya mazoezi ya mwili inasema ya kwamba huwezi kutengeneza six park kwa kufanya mazoezi ya aina moja pekee kila wakati, bali unaweza kutengeza six park kwa kufanya mazoezi ya aina tofauti tofauti. 

Kwa  muktadha huo kama kweli unataka kufanikiwa zaidi ya hapo ulipo sasa, unachotakiwa kufanya ni kuweza kutambua uwezo mwingine ambao mwenyezi Mungu kakuwekea ndani yako, ili uweze kujipatia mkate wako wa kila siku. 

Hata mwandishi mmoja aitwaye Antony Robbison aliwahi kuandika ya kwamba “if you do what you have done you will get what you always gotten” hii ikiwa na maana “kama utafanya mambo yaleyale ambayo umekuwa  ukifanya siku zote, utapata yale yele ambayo siku zote umeyapata”. Naomba urudie kusoma tena aya hii ili uielewe vizuri. 

Kwani aya hiyo ipo wazi kabisa kama umezoea kufanya mambo yale yale kwa njia ile ile basi matokeo yake, yatakuwa ni yaleyale. Hivyo ili uweze kupata matokeo ya iana tofauti  na uliyoyazoea, unachotakiwa kufanya kubomoa uzio wako wa kufikiri kwa kuanza kubadili ratiba ya kutenda mambo yako ya msingi. Lakini pia ongeza uzio wa kufanya mambo yako  kwani binafsi naamini una kitu kingine cha kufanya zaidi ya hicho ambacho unakifanya. 

Mwisho nimalizie makala haya kwa kusema ukitaka kwenda mbali zaidi katika mambo yako ya msingi acha kujenga uzio ambao utakufanya ushindwe kuona fursa nyingine,  bali unachotakiwa kufanya ni kubomoa uzio huo ili uweze kuona fursa mbalimbali ambazo zimejificha, kwani pindi unavyoacha ukuta huo ni kule kutengeneza uwezo wako wa kulalamika, na mwisho wa siku kuelekea jehenamu ya umasikini. 

Narudia kwa kusema tena pale unaposhindwa kujiongeza ni kutengeneza jehanamu ya umaskini. Usiogope na kusema afisa mipango anakutisha hapana,  ila kazi yangu ni  kukwambia ukweli ambao upo wazi, kwani nafasi uliyonayo sasa unachotakiwa kufanya ni kuwaza ni namna gani utaweza kufika mbali zaidi. 

Kwani umuhimu wa kujiongeza kunamsaidia mtu kuweza kuwa milango mingi ya kuweza kufanikiwa zaidi. Pia faida nyingine ya kujiongeza humsaidia mtu kuweza mbunifu zaidi kwa kile akifanyacho. Na ubunifu humsaidia mtu aweze kujilikana na ukijulikana ndo mwanzo wa mafaniko yenyewe. Mpaka kufikia hapo sina la ziada naomba kazi ibaki kuwa kwako kwa kuamua kwenda kuyatekeleza hayo ambayo nimekwambia. Asante.Ni wako katika ujenzi wa mafaniko. 

Jumatatu, 15 Januari 2018

Sababu

Sababu kuu 7 za kwanini kila mwanaume anahitaji mwanamke sahihi

Muungwana Blog 5 · Yesterday



Kwangu kipindi ambacho kilinivutia sana ni kipindi cha kampeni za uchaguzi nchini Marekani. 

Ni pale Obama akiwa katika kampeni kwenye moja ya majimbo kugombea duru ya pili ya uraisi aliposimamisha hotuba yake na kutambua uwepo wa mkewe Michelle. 

Obama alisema, "Mke wangu amekuwa bega kwa bega na mimi tokea niko chuo, kuna kipindi nilishindwa kulipa ada ila yeye ndiye aliyenilipia" 

Obama akaenda mbali zaidi na kukiri mbele ya jamii ya kimataifa kwamba asingekuwepo hapo alipo kama sio mke wake Michelle. 

Hivyo basi, nashauri kwamba mwanamke ambae mwanaume atakua nae huenda akawa chachu ya mafanikio na baraka kwake au anaweza akamrudisha nyuma kabisa katika mipango yake. 

Sababu kuu 7 za kwanini iwe isiwe mwanaume lazima upate mwanamke alie sahihi. 

1. Kila mwanamke anao uwezo wa kukuridhisha kimapenzi ila mwanamke sahihi na bora pekee ndiue anaeweza kuku-challenge kiakili na kuwa 'intellectually inspired'. 

2. Mwanamke yeyote anaweza kukuteka kihisia, ila yule sahihi pekee ndiye mwenye uwezo wa kukuteka kiroho na ukamtumikia Mungu wako. 

3. Mwanamke yeyote anaweza akakushawishi muandike mpango wa harusi (wedding plan), ila mwanamke sahihi peke yake ndie mwenye uwezo wa kukuandikia na kukushauri mpango wa biashara (business plan) 

4. Kila mwanamke anaweza akakubusu tena 'French kiss' ila mwanamke bora pekee ndio mwenye uwezo wa kukutamkia maneno yaliyojaa busara na hekima. 

5. Kila mwanamke anaweza akakupenda sana tu tena kama una pesa, ila mwanamke aliye bora pekee ndiye anaeweza kusimama na wewe hata kukuinua pale utakapokuwa huna kitu. 

6. Mwanamke yeyote anao uwezo wa kukushibisha kwa kukupikia chakula kitamu, ila mwanamke bora pekee ndio mwenye uwezo wa kukulisha chakula cha ubongo. 

7. Kila mwanamke anao uwezo wa kukushawishi chumbani ila mwanamke bora pekee ndio mwenye uwezo wa kukushawishi umrudie Mungu wako. 

Mwisho ngoja nihitimishe kwa kusema hivi ukisoma vitabu vya kihistoria kuhusu Winstom Churchhill mpaka Abraham Lincoln, na kutoka kwa Nelson Mandela mpaka kwa Martin Luther King Jr lao moja kwamba “No matter how strong a Man is, he is only as strong as the Woman he marries” Kwa tafsiri yangu ya kuunga unga isiyo sahihi sana Wanamaanisha "haijalishi ni kwa kiasi gani mwanaume una nguvu, nguvu zako zina athiriwa kwa kiasi kikubwa na mwanamke utakaemuoa"

Jumatatu, 8 Januari 2018

King mafla misemo ya ukweli

M


MandagoJF-Expert Member

#1Oct 5, 2010Joined: Feb 8, 2008Messages: 238 Likes Received: 80 Trophy Points: 45

Baadhi za Hekima na Methali za Kiarabu

1) Si vigumu kujitolea kwa kumsaidia rafiki yako,lakini ni vigumu kupata rafiki ajitolee kwa ajili yako.

2) Usiache ulimi wako ukafuata macho yako kwa kueleza aibu za watu, kumbuka kuwa watu nao wana macho na ulimi kama wewe.

3) Mambo yasiyokuwa na umuhimu huzungumzwa kwa muda mrefu kwani sote tuna yafahamu kuliko mambo muhimu.

4) Ikiwa una mikate miwili kula mmoja na mwingine utowe sadaka.

5) Mtu akisifiwa watu wachache huamini,lakini akikashifiwa wengi huamini.

6) Hakuna mtu ambaye hakufanikiwa kabisa,bali ameanzia na sifuri akabakia hapohapo. 

7) Binaadamu ambaye amefaulu ni yule anaye nyamaza kabla ya watu hawaja ziba masikio yao, na anafunguwa masikio yake kabla ya watu hawajafunguwa midomo yao. 

8) Kabla ya kuzungumza chaguwa neno la kusema, na uchukuwe muda wa kusema ili maneno yako yachipuwe kama linavyo chipuwa tunda.

9) Jihadhari na mtu ambaye ni mkarimu ukimdharau,na mtu mbaya ukimkarimu,na mwenye akili ukimkosowa na mjinga ukimrehemu.

10) Ukifikia kilele mwangalie jambazi ili upate mtu wa kukusaidia,na angalia mbinguni ili Mwenyeezi Mungu akuweke imara usianguke. 

11) Si kufaulu kugunduwa mambo wanayo yapenda watu,lakini kufaulu ni kuwa na ujuzi wa kuwafanya watu wakakupenda.

12) Shujaa anaye jitahidi kutatuwa matatizo yake,anafaidika na uwezo wake

13) Ukipanda jabali angalia kilele chake,wala usiangalie upande wowote na ulipande kwa makini,wala usiruke ukavunja mguu wako.

14) Shujaa ni yule ambaye anauwezo wa kukuza ujuzi wake,na kuweza kukuza ujuzi wa watu na pengine kuwabadilisha.

15) Usiache utajiri ukakufanya ukakosana na watu,kwani kuwa pamoja na watu ndio njia ya kuupata utajiri.

16) Badali ya kukaa na kutukana kiza,jaribu kutengeneza umeme. 

17) Ukitabasamu tabasamu kwa mtu masikini, kwani kunakuongezea malipo mema kwa Mwenyeezi Mungu.

18) Mwanamke humsubiria mume wake kwa umasikini wake,ubaya wake na kutokumjali kwake ,lakini hamsubirii kwa tabia mbaya yake.

19) Mtoto ni kama udongo(wa ufinyanzi) tuna mlea kwa jinsi tunavyo ona sisi. 

20) Watendee watu kama wao ni binaadamu si kwa sura zao wala pesa zao wala vyeo vyao. 

21) Uzuri wa mtu ni ndani ya nafsi yake,si sura yake. 

22) Ukisema neno litakumiliki,na usipolisema utalimiliki.

23) Anaye ishi na sura mbili,hufa bila ya sura

24) Adui yako akikuomba ushauri mpe nasiha,kwani ukimpa ushauri ataondosha uadui wake kwako na kukusaidia.

25) Ukizungumza wakati ukiwa na hasira,utasema neno ambalo utajutia maisha yako.

26) Usijadiliane na mtu mjeuri wala asiyekuwa na haya, kwani jeuri hutomuweza na asiye na haya atakuudhi.

27) Tabia njema ina sitiri mambo mengi mabaya,na tabia mbaya ina ziba mambo mengi mazuri.

28) Mwenye kumuamini Mwenyeezi Mungu humpa,mwenye kutawakal kwake humtosha,mwenye kumuogopa huacha aliyo yakataza na mwenye kumjuwa humuenzi.

29) Kunyamaza ni dalili ya kukubali jambo.

30) Jihadhari na ulimi wako,usiiponze shingo yako. 

31) Fimbo ya muongo ni fupi.

32) Si kila wakati mtu husalimika na jirani.

33) Ulimi wako ni kama farasi wako,ukiuchunga vizuri nao utakuchunga na ukiuachia nao utakuponza.

34) Ndege mmoja aliye mkononi mwako ni bora,kuliko kumi waliyoko katika mti.

35) Kila kimya kina jambo lake.

36) Ukitaka kutiiwa,amrisha mambo yanayo weza kufanywa.

37) Wezi wawili wakigo mbana ,vitajulikana vitu vilivyo ibwa.

38) Jihadhari na shari hata kwa mtu uliye mfanyia mema.

39) Upanga umeshinda kanuni.

40) Mwanzo wa mavuno ni tone la mvuwa.

41) Kuwa na haya ni katika imani.

42) Mazungumzo mazuri huwa mafupi na yanayo eleweka.

43) Mwaka ni kama siku mbili,siku kupata na siku kukosa.

44) Huto pata hasara ukimshauri mtu.

45) Haraka hutokana na shetani.

46) Kila kiongozi,na hotuba yake.

47) Mwenye kuingilia jambo lisilo muhusu,husikia yasiyo mridhisha.

48) Wakati ni kama upanga usipo ukata utakukata.

49) Haurushiwi mawe,isipokuwa mti wenye matunda.

50) Mwenye kuwachunguza watu hufa kwa kiroro(hamu). 

51) Watu bora zaidi ni wale wanao towa daawa kwa vitendo vyao kabla ya maneno yao.

52) Uwezo wa kuathiri nyoya za watu,na kupata pendo lao la kweli hutuletea furaha kubwa katika maisha yetu.

53) Nia nzuri ni kufanya ujuzi wa kuwafanyia watu mambo ya ibada,kwani hukukurubisha na Mwenyeezi Mungu(huwa karibu na Mweyeezi Mungu) 

54) Usifikirie watu wote ni sawa,kwani kuna watu wenye tabia tofauti kuliko aina za rangi

55) Zungumza na watu kwa mambo ambayo wana penda kuyasikia,siyo kwa mambo ambayo unaya penda wewe.

56) Mkutano wa kwanza huchukuwa asilimia thamanini ya tabia ya mtu anavyo onekana, wafanyie watu wote kama kwamba huo ni mkutano wa kwanza na wa mwisho kati yenu.

57) Kuijuwa tabia ya mtu ndio kuna kupa uwezo wa kupata pendo lake.

58) Kila mtu ana ufunguo wake,kwa kujuwa tabia ya mtu ndio kujuwa njia ya kuelewana nae.

59) Binaadamu hufanya mambo yote kwa moyo wake siyo kwa mwili wake.

60) Ukimiliki nyoyo za watu hupendeka

61) Mtu kujitahidi kutoingilia mambo yasiyo muhusu ni vigumu lakini humpumzisha.

62) Kuwa kama nyuki anatuwa juu ya kitu kizuri na kujiepusha na kitu kibaya, usiwe kama inzi kutuwa juu ya vidonda.

63) Huwezi kula asali bila ya kuvunja nyumba ya nyuki.

64) tukifanya watu wajuwe kwamba tunaangalia mazuri yao kabla ya mabaya yao watakubali kupokea nasiha.

65) Ni bora mtu kujuwa kosa lake si sharti kulisahihisha mbele ya watu.


R

ReasoningMember

#2Oct 6, 2010Joined: Mar 7, 2009Messages: 57 Likes Received: 0 Trophy Points: 0

Asante Mandago. Hakika ni misemo iliyojaa hekima sana. Chukua tano!!!


myao wa tunduruJF-Expert Member

#3Oct 6, 2010Joined: Mar 9, 2010Messages: 613 Likes Received: 20 Trophy Points: 0

ubarikiwe mkuu Mandago....nimejifunza kitu


MahmoodJF-Expert Member

#4Oct 7, 2010Joined: Feb 9, 2008Messages: 7,851 Likes Received: 1,336 Trophy Points: 280

Asante sana ndugu Mandago kwa haya maneno yenye hekima kubwa, nimejifunza mengi katika meneno haya ya hekima.


(You must log in or sign up to reply here.)

 Facebook


 Twitter


 LinkedIn


 Google+


 Pinterest


 Email


WHO ARE WE?


JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic. You are always welcome!

Read more...


WHERE ARE WE?


We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually. For anything related to this site please Contact us.

Contact Us Now...


DISCLAIMER


JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

Read more...


FORUM RULES


JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you. You MUST read them and comply accordingly

Read more...


PRIVACY POLICY


We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one. Read our Privacy Policy.

Proceed here...



Contact Us


Help


Jumamosi, 16 Desemba 2017

NINGEMSIKILIZA

Mimi na yeye tulikuwa na harusi nzuri. Tulitegemea ndoa yetu itadumu kwa muda mrefu. Tulikuwa na ndoto na mipango mikubwa. Oh tulikuwa na mawazo makubwa mpaka pale nilipopotea njia...


Mungu alinibariki, yes alinibariki sana. Mke mzuri mikononi mwangu ambae kila mwanaume angetamani kuwa nae. Watoto wazuri watatu wenye afya na kazi iliyokua ikinilipa vizuri.


Nilikuwa nalipwa mshahara mzuri, hivyo nikafikiri namna ya kuufurahia zaidi. Taaratibu nikaanza kujisogeza club na pubs mbalimbali nikinywa hata bia moja.


Bia moja zikawa mbili, zikawa tatu...pombe akawa rafiki yangu mpya. Kuniona kwenye Bar ikawa kama dini yangu. Nilikuwa na pesa hivyo pombe ilitakiwa iniabudu.


"Mhudumu, wazungushie wale wote" nilikuwa nikipiga kelele za kilevi kila nilipokuwa Bar. Walevi wakaanza kunifurahia...nikawa celebrity Bar zote hot zilizopo mjini, kuanzia Sewa Bar, Catalunya, hata Corner Bar...


Lakini nyumbani nilikuwa mbogo, mke wangu akawa akiniuliza nakuwa mtu wa aina gani? Alikuwa akilia..akinililia jinsi nilivyobadilika...
.
Mke wangu alikuwa akinililia niwahi kurudi nyumbani, lakini sikuwa namsikia. Unajua nini? Nilikuwa nawaza kuwa nimeshamuoa kwaiyo haina haja ya kum-please!


Nilikuwa naona kama ananiwekea kiwingu tu, wanawake wa Bar walikuwa wakinipenda. Mke wangu aliniona nimekuwa kama mtoto mdogo na mimi niliona mke wangu anajiona kama mama yangu kunizuia starehe zangu..!


"Unaanzaje kumruhusu mwanamke akwambie nini cha kufanya? Nani kichwa cha nyumba? Mzibe mdomo wake.." Marafiki zangu wa Bar walinishauri hivyo.


Niliwasikiliza washikaji wangu kwa sababu walikiwa wakinifanya nijione kama mfalme, wakati nyumbani nilikuwa nashindwa kutimiza majukumu kama mfalme kwa malikia mke wangu.


Nilikuwa mume na baba niliefeli kwenye majukumu yangu. Nilichokua najua ni kupiga makelele Bar kama mbwa na kufukuzia wanawake wa Corner Bar na kwingineko waliojikatia tamaa.


Usiku baada ya usiku silali nyumbani. Mke wangu akaanza kukata tamaa..akaacha kunitafuta..mke mwenye heshima zake humtafuta mfalme wake aliko, sio mbwa apigae kelele kwenye Bar..akaanza kujifunza kuishi bila mimi.


Alichoka kuniambia kwamba napoteza pesa, pesa zetu, naharibu ndoa yetu, naharibu nyumba yetu..wale wanawake waliojikatia tamaa wakawa waki-sex na mimi na kunila pesa zangu huku wengine wakiniibia pale napolewa.


Washikaji zangu nao wakawa wakinitumia mimi kama mgodi wa pesa kujihudumia mahitaji wanayotaka..nilikuwa nahitaji kuabudiwa na kunyeynyekewa..pedeshee mtoto!!


Lakini nyumbani nilikuwa mbahili, zaidi ya milioni 50 zilinipotea kwa mambo ya kipuuzi. Niliwapa faida kiwanda cha Bia, lakini hata kuwanunulia nguo wanangu nilishindwa.


Nilipewa onyo za kutosha ofisini kwa sababu ya kwenda kazini huku nimelewa, nikawa nafanya kazi chini ya kiwango..mara tatu nimesababisha ajali..kwa kuendesha huku nikiwa nimelewa..


Wala sikutilia maanani kuonywa na wakubwa wangu wa kazi, kama nilivyokua simtilii maanani mke wangu..


Mtu yeyote aliekuwa anakuja kwa nia ya kunitenganisha na pombe akawa ni adui yangu mkubwa..nikawa na maadui wengi..


Mke wangu akiwa adui yangu namba moja. Mke wangu, mama wa watoto wangu..mwanamke niliyemuoa naishia kumpa stress na kupoteza uzuri wake waote..alishindwa kuvumilia zaidi...pale nilipoanza kuja na malaya ndani ya nyumba yetu...tena mbele ya watoto...


Akabeba mabegi yake, akachukua watoto wetu na kuondoka na kuniacha...


Nikafukuzwa kazi, nikanyang'anywa nyumba ya kampuni, nikanyang'anywa gari na mali zote za kampuni....


Nikapoteza marafiki, nikapoteza hata wale wanawake waliokuwa wakinipa sex..nikapoteza na heshima yangu..na ndoto zangu zote..lawama ni kwa pombe!


Lakini hapana, lawama si kwa pombe, najilaumu mwenyewe, najilaumu kwa msimamo wangu wa kipuuzi na najilaumu kutomsikiliza mke wangu na kuwa upande wa marafiki feki ambao wapo unapokuwa na pesa tu.


Sasa hivi niko hapa kitaa, Bar ya mtaani tu, nimepanga chumba kimoja kisichokua na umeme na nadaiwa kodi ya miezi mitatu..niko nimelewa, pombe za kienyeji nikiimba nyimbo za dini kujifariji..


Bado nashangaa nitapata wapi pesa ya kodi, nitapata wapi pesa ya matibabu kutibu madhara ya pombe kali iliyoharibu INI langu.


Niko hapa, mikono yangu inatetemeka.
Nimeshika glass ya pombe ya kienyeji.
Pombe imekua ndio kila kitu kwangu japo ya maladhi niliyonayo.


Ghafla namuona mke wangu anaonekana kwenye TV iliyopo kwenye kilabu cha mama Muuza. Anafanyiwa interview..Kampuni yake ya vipodozi inafanya vizuri..


Anaongelea biashara, GDP ya nchi na ajira kwa vijana na wanawake..


Na mimi niko hapa kwa mama muuza, sina hata mia..pombe ya kienyeji nimekopa....


"Mama muuza eeh ongeza sauti ya tv..!!" Napiga kelele kwa muuzaji.


Mke wangu yuko mbali, wote tungekua mbali kama ningemsikiliza...


"Aah mama muuza kama vipi zima TV, au badilisha channel.." Naropoka kilevi!
___________________________


Wanaume, tujifunze kusikiliza wake zetu. Wameumbwa kwa ajili ya kutusaidia..tuache watusaidie..wao pekee ndio wenye best interest na sisi kwenye mioyo yao...


Toa Maoni yako hapa chini:


Njia 10 Za Kupunguza Magonjwa Ya Mlipuko Wa Kuku

Njia 10 Za Kupunguza Magonjwa Ya Mlipuko Wa Kumgisha Blog · 8 hours ago




Mlipuko wa magonjwa ni moja ya sababu za hasara kubwa kwa wafugaji na vifo vinavyotokea kwa wakati mmoja. Pindi mfugaji anapokumbwa na janga la vifo vya ndege, kabla ya kufikia mwisho wa mzunguko wa uzalishaji hivyo basi asitarajie kupata faida nzuri mara baada ya mauzo. 
Hasara itokanayo na vifo inaweza kuepukika au kupunguzwa na kutokea kwa kiasi kidogo. 

Hili linawezekana, ifuatayo ni namna ya kufanikisha hilo;- 

1. Osha vyombo vya maji kila wakati na mwaga maji yaliyobaki. 
Hakikisha unamwaga maji yaliyosalia mbali na kuosha chombo na sabuni kila siku, weka maji safi yasiyo na dawa na wala usitumie maji ya mto au yale usiyoyajua chanzo chake. Kama utaweka maji dawa basi tumia ‘vitamini’ muhimu kama ‘vitalyte’ ambazo zinasaidia kuua vijidudu. 

2. Wape maji kabla ya chakula. 
Ndege wapo tofauti na binadamu au wanyama wengine. Hakikisha unawapa maji kabla ya chakula hasa kama unatumia maranda, hii ni kuhakikisha hawakanyagani wanapogombania chakula sehemu moja. 

3. Usiwape chakula chenye uvundo. 
Ni hatari sana kuwapa ndege/kuku wako chakula chenye ukungu, ni kama kuwalisha sumu. Ukungu au uvundo huwafanya kuku waugue kirahisi sana au kuwasababishia madhara mengine kiafya. 

4. Fuatilia kwa makini ratiba za chanjo na tiba. 
Mfugaji unatakiwa kupata tiba na chanjo sahihi kwa ndege unaowafuga. Kuchanja ndege kutasaidia sana kuimarisha kinga yao dhidi ya magonjwa hatari kama kideri, ndui, gumboro na mareksi. Dawa kama vile za minyoo na antibayotiki ni muhimu sana kwenye afya ya kuku na ndege wengine. 

5. Nunua na fuga vifaranga wenye afya njema. 
Matatizo mengi ya afya ya ndege au kuku ni matokeo  ya maisha duni ya awali ya kuku hao au huwa wanarithi. Itambulike hivi, baadhi ya ndege/kuku hurithi afya mbovu kutoka kwa wazazi wao. Hata hivyo baadhi ya watotoleshaji pia wanafuga kuku ambao wana afya mbovu na hivyo huuza vifaranga au mayai dhaifu na waathirika na hivyo mnunuzi anajikuta ananunua matatizo. 

6. Zuia mkusanyiko wa hewa ya ammonia. 
Maranda yakikaa muda mrefu bandani, hufanya hewa ya ammonia kuzalishwa kwa wingi, hewa hii hufanya ndege wapaliwe hadi kufa. Kila mara ondoa maranda mabichi au yaliyovunda na weka mengine haraka iwezekanavyo ili kuepuka vifo vitokanavyo na kupaliwa au magonjwa ya mfumo wa hewa. 

7. Zuia panya na vicheche. 
Banda la ndege linatakiwa lisiruhusu panya au wanyama wadogo jamii ya kicheche kuingia ndani, na ndege wa mwituni kwa kuweka nyavu au kupulizia dawa, ikiwa watapata upenyo wataua na kula ndege/kuku wako na kuacha vimelea vya magonjwa wanapokula vyakula au kunywa maji ya ndege wako. 

8. Zingatia usafi na usalama. 
Kipengele hiki cha usafi na usalama ni kipana  ila unachotakiwa kufanya ni kuzingatia usafi nje na ndani ya banda. Unatakiwa ukamilishe usalama wa afya ya ndege/kuku wako kila wakati, jambo ambalo wafugaji wengi hutekeleza pindi wanapo shitukizwa na mlipuko wa magonjwa. 

9. Wape chakula cha kutosha. 
Ndege kama walivyo wanyama wengine, hawawezi kukua na kuzalisha vizuri endapo wanapewa chakula duni na kidogo. Chakula bora ni msingi imara  na ni kinga kwani chakula duni hupelekea uzito kupungua na kinga kuwa chini na hivyo hufa mapema. Jitahidi wape kuku chakula cha kutosha ila usiwazidishie. 

10. Wakinge dhidi ya baridi kali. 
Baridi kali ni adui kwa afya ya wanyama, ndege na binadamu. Jaribu kila uwezavyo kuwakinga kuwakinga ndege wako na baridi kali kwani inaua haraka sana kama sumu. Wawekee chanzo cha joto wakati wa baridi au jenga banda ambalo halipitishi baridi kali. 

Hizo ndizo njia muhimu ambazo ukiwa mfagaji unazoweza kuzitumia ili kukinga magonjwa yanatokanayo na kuku.

Kama Unaogopa Kufanya Kitu Hiki, Sahau Kuhusu Mafanikio Katika Maisha Yako Yote

Kama Unaogopa Kufanya Kitu Hiki, Sahau Kuhusu Mafanikio Katika Maisha Yako Yote

Kamgisha Blog · 5 hours ago



Fikiria kila unachokijua na kukikumbuka kuhusu mabadiliko unayotaka yawe katika maisha yako, halafu  uone ukweli huu  kama kweli nawe ni mmoja kati ya watu wanaotaka mafanikio au uko nje ya mstari wa mafanikio na pengine tu wewe hujijui. Kama kweli unataka mafanikio, ni kwanini  mara kwa mara umekuwa ukisita au kuogopa kufanya jambo ambalo lingeweza kubadili maisha yako na kukuletea mafanikio mkubwa? Hili ndilo tatizo walilonalo watu wengi wanahofia sana kufanya mabadiliko kwa namna moja au nyingine hata kwenye yale malengo waliojiwekea wao wenyewe kuna wakati huwa wanaogopa pia. 

Kimaumbile, kila binadamiu anahofia mabadiliko, lakini hofu ya mabadiliko inapozidi kuwa kubwa na kukuzuia kufanya mambo ya maana kwako, hofu hii  sasa hugeuka kuwa ni maradhi yanayokuzuia wewe kufanikiwa. Hebu fikiria tena, ni mara ngapi umekuwa ukitaka kufanya mabadiliko Fulani  katika maisha yako, lakini umekuwa ukijikuta ukishindwa kufanya hivyo kutokana na kuogopa kufanya vitu Fulani? Ni mara ngapi umekuwa ukitaka kuingia kwenye biashara lakini umekuwa na hofu nyingi zinakuzuia? Hivi ndivyo ilivyo mabadiliko huogopwa, wakati mwingine bila sababu ya msingi. 

Wengi wetu kutokana na kuogopa mabadiliko, hujikuta ni watu wa kutoa sababu ambazo hata hazina mashiko zinazosababisha wao washindwe kutekeleza malengo na mipango waliojiwekea. Utakuta mtu anakwambia  hawezi kufanya biashara ni kwa sababu hana mtaji, ukija kuchunguza kidogo utagundua kuwa hiyo ni sababu ambayo amekuwa akiitoa kwa muda mrefu, iweje kila siku mtu huyohuyo awe hana mtaji tu. Kama uko hivi una hofu tu hata kwa vitu vidogo ambavyo ungeweza kuvifanyana , tambua kuwa kuanzia sasa unaye adui mkubwa ndani mwako anayekuzuia kufanikiwa. Na unapoogopa kufanya mabadiliko ambayo unaahitaji sasa ili ufanikiwe, sahau kuhusu mafanikio katika maisha yako yote. 

Tatizo kubwa utakalokuwa nalo linalosababishwa na hofu hii ya kuogopa kufanya mabadiliko ni lazima utakuwa mtu wa kutaka mafanikio ya harakaharaka. Watu wengi wenye mawazo ya kutaka kufanikiwa leoleo hata kama wameanza biashara leo, wengi wao huwa wana hofu hii kubwa ya mabadiliko ndani mwao, unaweza  kufanya utafiti mdogo utagundua ukweli huu ulio wazi. Hawa ni watu ambao kiuhalisia hawaijui wala kuiamini subira ndani mwao, bali ni watu wakutaka mfumo wa maisha uwe ambao unaanza leo biashara na wiki ijayo uwe tajiri ni kitu ambacho hakiwezekani kabisa. 

Hivi ndivyo walivyo watanzania wengi wanaogopa mabadiliko na kuamini katika miujiza, sio katika wao wenyewe kutenda na kuona matokeo.  Hebu jaribu kukagua maisha ya walio wengi utakuja kugundua ukweli huu ni watu wanaofikiria sana leo, sasa hivi, siyo baadaye. Hata malengo yao ni ya karibu sana na hawataki shida, wanataka wafanye leo, wamudu leo na kila kitu kimalizike leo. Sijui kesho watafanya kitu gani? Ukimwambia mtanzania aanzishe mradi ili aje faidi baada ya miaka 10 kutoka sasa kwanza atakushangaa, kisha atakucheka we hadi mbavu zimuume. Anataka leo hata kama ni kwa miujiza. 

Ndiyo maana wengi kati ya Watanzania hawana malengo, wanaishi tu na kutawaliwa na hofu za mabadiliko. Kuweka malengo siyo sehemu ya maisha yao, kwani malengo yanataka mtu mwenye subira, mtu anayeamini kwamba maisha ni kuanguka na kusimama. Wanachojua kikubwa ni kulalamika na kulaumu, kuponda na kukejeli, kwa sababu wao wamekata tamaa bila kujijua. Ndiyo maana ni watanzania wanne tu kati ya kumi ambao wanafanya kazi, wanatoka jasho na wanaweza kusubiri bila kukata tamaa, wengine waliobaki wanasubiri ujanja ujanja tu ilimradi wafanikiwe hata kama ni kwa kufanya uhalifu wa aina yoyote. 

Ni watu ambao wanataka kuishi kihadithi, wawe na pete ambayo wanaweza kuiamuru iwape wakitakacho na wakipate. Maisha ni ya kibunuasi- abunuasi tu, watu hawa kwao mabadiliko ni kitu kigumu sana kwao na kinaogopwa kweli. Kama unataka mafanikio ya kweli yawe kwako, unatakiwa kubadilisha fikra za zako na kuamua kukubali kuwa mafanikio yanahitaji mabadiliko makubwa sana ambayo wewe mwenyewe unatakiwa uyafanye kwa kujitoa hasa. Acha kuwa na hofu zisizo na maana zinazokuzuia wewe usifanikiwe, chukua hatua katika maisha yako, kuyafikia maisha unayoyataka. 

Jumapili, 5 Novemba 2017

King mafla misemo ya ukweli




NgongosekeJF-Expert Member

#1Nov 15, 2014Joined: Jan 1, 2012Messages: 3,212 Likes Received: 18 Trophy Points: 135

Funguo nimezipenda

Jihadhari na machozi namna tatu:
1-Chozi la aliyedhulumiwa
2-Chozi la yatima
3-Chozi la baba na mama yako
Moja ya machozi haya yakitiririka, umejifungulia jahannam
🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐

Usimuumize aliyekupita umri, na wala usimkatize.. siku moja utakuwa kama yeye
🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐

Kufanya utani kwa maandishi kunaweza kufahamika vibaya kwa sababu ya kukosekana ishara ya uso na mikwaruzo ya sauti.. basi kuwa makini katika kuchagua maneno yako, kwani wengi wa watu ni wanatafsiri vyengine
🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐

Utamu wa maisha ni kuishi kwa staili yako, na si staili ya wengine
🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐

Ni kweli kwamba maji yanarudi kwenye mkondo wake, lakini yakirudi yanakuwa hayafai kuyanywa
🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐

Usijaribu kufuatilia kila kitu, huenda ukafahamu sivyo na ukawapoteza wengi walio karibu yako kwa sababu ya fikra zako.. jambo la kufanya; kuwa na dhana njema kwa walio karibu nawe
🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐

Watu wengi wanazungumzia kutenda na hawafanyi lolote.. na wengine hawasemi watakalofanya na wanafanya na kupata wanayotaka
🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐

Hakuna tofauti kati ya rangi ya chumvi na ya sukari.. vyote viwili ni rangi moja.. lakini tofauti utaijuwa baada ya kujaribu! halikadhalika wanadamu
🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐

Wengi wanaoongelea aibu za watu ni watu ambao hawaangalii aibu zao kubwa, miongoni mwa hizo ni vile wao kuhadithia aibu za watu
🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐

Marafiki hawabadiliki bali sisi tunafanya haraka kuwaita baadhi ya watu marafiki
🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐

Baadhi ya watu watakuacha, lakini hiyo si mwisho wa kisa cha maisha yako, bali ni mwisho wa nafasi yao kwenye kisa chako si zaidi
🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐

Hutaweza kubadilisha umbo lako ili uwe mzuri zaidi kwenye macho ya watu, lakini unaweza kudhibiti tabia yako na kuipendezesha adabu yako ili uwe mzuri kwenye macho ya watu
🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐🔐

Sisi ni jamii tukitaka haraka tunasema jambo jema ni bora lifanywe haraka.. na tukitaka kuchelewesha tunasema kuchelewa kuna kheri yake.. masuala ni mizaji, si zaidi


- 1 people like


K

kibobori.1Senior Member

#2Nov 15, 2014Joined: Nov 7, 2014Messages: 168 Likes Received: 0 Trophy Points: 0

Kweli kabisa mkuu


- 1 people like


promisemeJF-Expert Member

#3Nov 15, 2014Joined: Mar 15, 2010Messages: 2,715 Likes Received: 29 Trophy Points: 135

Mkuu hayoo machozi nna ya ogopa! Haswa ya yatima kwanza nawaonea huruma..


NgongosekeJF-Expert Member

#4Nov 15, 2014Joined: Jan 1, 2012Messages: 3,212 Likes Received: 18 Trophy Points: 135

promiseme said: 

Mkuu hayoo machozi nna ya ogopa! Haswa ya yatima kwanza nawaonea huruma..


Inabidi uogope yote na wazazi pia na ya dhulma usisahau


promisemeJF-Expert Member

#5Nov 15, 2014Joined: Mar 15, 2010Messages: 2,715 Likes Received: 29 Trophy Points: 135

Ngongoseke said: 

Inabidi uogope yote na wazazi pia na ya dhulma usisahau


La wa zazi alhamdulillah najitahidi sana na uzuri wazee Wangu wametulea malezi ya dini najua umuhimu wa wazazi, na bila kusahau dhulma, sababu yakusema yatima nalea watoto wa Mtoto wa shangazi yangu wako 3 sasa 1 Kati Yao nimkorofi kupitiliza ananisugua roho Mpaka nalia kwakusema....


N

NandoJF-Expert Member

#6Nov 15, 2014Joined: Oct 5, 2014Messages: 4,783 Likes Received: 1,453 Trophy Points: 280

Maneno yako yapo vzuri yamenigusa.


(You must log in or sign up to reply here.)

 Facebook


 Twitter


 LinkedIn


 Google+


 Pinterest


 Email


WHO ARE WE?


JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic. You are always welcome!

Read more...


WHERE ARE WE?


We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually. For anything related to this site please Contact us.

Contact Us Now...


DISCLAIMER


JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

Read more...


FORUM RULES


JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you. You MUST read them and comply accordingly

Read more...


PRIVACY POLICY


We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one. Read our Privacy Policy.

Proceed here...



Contact Us


Help